Monday, October 24, 2011

Waraka wa Kinabo:Kwa Serikali hii,daima tutaomboleza uzembe

Na Edward Kinabo

NIMERUDI tena, kwa uchungu na hisia nzito. Mungu azilaze mahali pema peponi roho za Watanzania wenzetu waliopoteza maisha kwenye maafa ya mv Spice Islanders. Mungu azijaze moyo wa uvumilivu na ujasiri familia zao, ndugu, jamaa na rafiki zao wa karibu, hususan katika kipindi hiki kichungu.

Wapo watakaosema “ajali haina kinga”, na wapo watakaodiriki kusema, “Wamekufa kwa sababu hiyo ndiyo siku yao waliyoandikiwa na Mungu”, kwamba “kazi ya Mungu haina makosa”. Fikra hizi, zinazoonekana kuwa za kiungwana na za kumcha-Mungu, ndizo zinazoifanya Serikali hii ya kizembe kuendelea na uzembe wake na kusababisha wananchi wengi kupoteza maisha katika mazingira ya kizembezembe, uzembe ambao na sisi kwa kujisahau, tumekuwa tukiulinda kwa kuwa na fikra na misemo kibao ya kumsingizia Mungu.

Ni kweli, kazi ya Mungu haina makosa, lakini kazi ya Mungu haipaswi kuingiliwa na mkono wa binadamu. Mungu wetu hawezi kuwa mzembe kama viongozi wa Serikali ya CCM, na ile ya Umoja wa Kitaifa kule Zanzibar. Na hata ikimlazimu kuwachukua watu wake, hana sababu ya kuwachukua kizembezembe.

Najua, wapo waungwana wengine watakaosema kuwa si ustaarabu kuchanganya siasa na suala la ajali iliyopoteza maisha ya watu. Lakini tunawezaje kupuuza nafasi ya siasa katika hili, ikiwa siasa za ghiliba ndizo zilizopachika viongozi wazembe wanaosababisha maafa yasiyokwisha kwa taifa?

Utakuwa ni ustaarabu wa kipuuzi ikiwa tutabaki kulialia tu na kuomboleza mauti yatokanayo na Serikali ya kizembe, bila kuchukua hatua za haraka dhidi ya serikali hii. Nani alijua kuwa baada ya maafa ya meli ya mv Bukoba, kungetokea tena maafa haya ya MV Spice Islanders? Nani alijua kuwa baada ya milipuko ya mabomu ya Mbagala, kungetokea tena maafa ya milipuko ya mabomu ya Gongo la Mboto? Nani anajua kuwa kabla ya mwaka 2015, Serikali hii hii ya kizembe, itakuwa imesababisha tena maafa na mauti mengine kwa Watanzania?

Na nani anajua kuwa katika maafa na mauti yajayo kizembe, mmoja wa marehemu anaweza kuwa mimi au wewe?

Badala ya kumsingizia Mungu, tuchukue hatua. Kama nchi imelaaniwa, basi ni muhimu ikafanyika toba ya kitaifa, ili atunusuru na uzembe na nuksi zote (kama zipo) zinazosababisha mauti makubwa kwetu. Kinyume na hayo, tunapaswa kuanzisha vuguvugu lisilokoma la kunusuru uhai wetu na wa nchi yetu dhidi ya utawala wa kizembe, na si lazima kusubiri uchaguzi wa 2015.

Mauti ya kizembe hayasubiri chaguzi, yanatokea wakati wowote na yanaweza kutuchukua sote, wewe mimi au wapendwa na wapenzi wetu. Pima mwenyewe…
Mungu wetu hana sababu ya kuhangaika kujaza mizigo mingi na abiria wengi kwenye meli ili izame ndipo aweze kuwachukua watu wake kwa kuchomoa roho zao.

Na wala hana sababu ya kuwaua watu wake kwa mv Bukoba halafu tena aje awaue kwa MV Spice Islanders. Hapana, yote hiyo ni kazi ya binadamu wazembe waliopewa dhamana ya kulinda uhai wa binadamu wenzao. Mungu wetu akitaka kukuchukua anakuchukua tu, si mpaka asubiri meli zijaze watu kupita kiasi au zipate hitilafu.

Watanzania wenzetu zaidi ya 240, kama mimi na wewe, wamepoteza uhai kwa sababu tu meli ya mv Spice Islanders ilipakia mizigo na abiria wengi kupita kiasi, au ilipata hitilafu, na hivyo kuzama kwenye Bahari ya Hindi. Isingepakia mizigo na abiria wengi isingezama, au ingekaguliwa vizuri na kufanyiwa matengenezo ya kufaa kabla ya safari, isingepata hitilafu wala kuzama.

Kwa maana hiyo, maafa yaliyotokea yangeweza kabisa kuepukika kama vyombo vya Serikali hii, ikiwemo mamlaka za usafiri wa majini, vingekuwa vinatimiza wajibu wake bila kuzembea.

Itiliwe maanani kuwa meli hiyo ilizama majira ya saa 7 usiku, na abiria wengi walikuwa wakifanya jitihada za kujiokoa, lakini kwa sababu ya “uzembe”, vikosi vya uokoaji vilichelewa kutumwa eneo la tukio na matokeo yake vilifika saa 12 asubuhi, takriban saa tano baada ya ajali kutokea.Katika hali hiyo, abiria wengi ambao wangeweza kuokolewa walikuwa wameshapoteza maisha.

Katika moja ya maandiko yake kuhusu “Uzembe wa Serikali ya CCM”, Mwanaharakati, Erick Ongara, baada ya kutokea kwa maafa ya milipuko ya mabomu ya Gongo la Mboto, aliandika hivi, namnukuu kwa kirefu:
“Tunaandika kwa hisia nzito sana. Tumefikishwa mahala ambapo tunalazimika kuwalinda raia dhidi ya Serikali yao. Ni kama kuwatenganisha vitoto vya mnyama wa kufuga na Mzazi wao ili kuwaokoa wasiliwe. Serikali ya CCM ikitumia silaha yake kubwa ya maangamizi iitwayo “uzembe” imeua waajiri wake kwa mara nyingine tena.

Imewaua, ikawalemaza, ikaharibu mali zao na kuwapa athari hasi na za kudumu Watanzania huku ikiendelea kuwafukarisha. Serikali ya CCM imejingea utamaduni wa kuishi katika duara la uzembe. Yaani huwa inahaidi, haijali, haijifunzi, haitendi na inapumzika mda wote kisha duara la uzembe linaanza tena.

Baada ya maafa ya Mbagala, serikali ya CCM ilihaidi kwamba hali hii haitatokea tena, kisha haikujali kufuatilia ilichoahidi, haikutenda katika kudhibiti uwezekano wa hali hiyo kujirudia na hatimaye ikapumzika. Baada ya mwaka mmoja na nusu duara la uzembe lilianza tena na kusababisha milipuko ya mabomu kutokea kwenye kambi ya jeshi Gongo la mboto.

Gongo la Mboto imeshalipuka na tayari wameahidi, kisha hawatajali, hawatatenda, watapumzika na hatimaye wataua tena kwa staili nyingine ya kizembe na duara la uzembe litaanza tena mwanzo.

Mwaka 2006 taifa lilikuwa na changamoto kubwa sana ya umeme. Wakasema tuna dharura. Wakabuni kampuni ya uongo. Wakajilipa, wakatunga kesi,wakahakikisha wanashindwa na sasa wanataka tuilipe fidia kampuni hiyo.

Leo duara la uzembe limeanza tena. Kuna dharura ya kuliokoa taifa dhidi ya kiza totoro.

Baada ya mwaka 2006, waliahidi, hawakujali, hawakutenda,wakapumzika na leo tumerudi pale pale. Tuna dharura (wamekuja na mpango wa dharura).

Kwa serikali hii ya kizembe, Tanzania ndiyo imekuwa taifa pekee dunia, lenye dharura za kudumu.

Kinachoumiza, vifaa vinavyopaswakuwalinda raia ndivyo vinavyowaangamiza. Risasi za polisi wa Arusha zilipaswa kuwahakikishia ulinzi raia, lakini zikawaua kwa kuwa tu walikuwa wanatembea pamoja wakiwa wameshika vitambaa vyeupe.

Wakazi wa Mbagala na Gongo la Mboto wamepoteza maisha kwa mabomu ambayo yalipaswa kuwahakishia ulinzi. Wanakatwa kodi, silaha zinanunuliwa kisha zinaingizwa katika mfumo wa duara la uzembe. Wanaahidi, hawajali, hawatendi na hatimaye wanapumzika.

Kwa bahati mbaya sana umma nao una duara saidizi kwa duara la uzembe. Kuna duara la uovu. Serikali inapokosea na kushindwa kutekeleza wajibu wake katika kiwango cha kuhatarisha na hata kupokonya maisha yao, Watanzania huwa tunajadili, tunachambua, tunalalamika, hatuchukui hatua kisha tunapumzika.

Serikali ikilizua tena, huanza duara upya, wananchi watajadili, watachambua, watalalamika, hawatachukua hatua kisha watapumzika, na matokeo yake maafa mengine yataibuka tena kwa sababu ya uzembe.

Zipo sauti zinazotaka mkuu wa majeshi na waziri wa ulinzi wajiuzulu kama sehemu ya uwajibikaji. Ni kweli na ni sawa kwa kuwa ndio wao walioahidi,kisha hawakujali,hawakutenda na hatimae wakapumzika.

Ili kudhoofisha duara hatari la uzembe lazima waaachie ngazi kwa maana wameshindwa kubeba dhamana ya kulinda uhai wetu.

Lakini hiyo pekee haitoshi. Lazima kutokomeza kabisa duara la uzembe kwa kumwajibisha kiongozi wa juu anaelea duara hili (Rais wa Nchi).

Ili kuondoa duara la uzembe lazima kwanza tuondoe duara la uovu.Watu wa Misri hivi karibuni hawakutengeneza duara bali mstari. Walichambua, wakakubaliana, wakajikusanya, wakashinikiza na hatimaye kuvunja duara la maangamizi kwao, ambalo lilidumu kwa miongo kadhaa.

Tumeumia sana na tunawapa pole ndugu zetu kwa maafa wanayoyakabili. Inawezekana, timiza wajibu wako. Mwisho wa kunukuu.

Baada ya maafa ya milipuko ya mabomu Gongo la Mboto, duara la uzembe liliendelea tena, na serikali ya CCM ambayo wakati wa ajali ya mv Bukoba, iliahidi kuongeza usalama wa vyombo vya usafiri wa majini, ikafanya tena uzembe na kusababisha meli ya mv Spice Islanders kuzama baada ya kuiacha ipakie mizigo na abiria wengi kupita kiasi. Na sasa taifa linaomboleza msiba mzito, msiba wa kizembe.

Katika hali hii ya ajali za kizembezembe, ni dhambi kubwa kusema “ajali haina kinga”, au kusema “kazi ya Mungu haina makosa”. Mungu wetu si mzembe. Kwa serikali hii, daima tutaomboleza mauti ya kizembe. Ni wakati wa kuchukua hatua za haraka. Tutafakari kwa pamoja.

SOURCE: Tanzania Daima Newspaper, September, 2011

Waraka wa Kinabo:Ufunuo wa Chadema Musoma

Na Edward Kinabo

MAENDELEO ya kweli na ya haraka yanawezekana, ikiwa kuna serikali yenye viongozi waadilifu na wanaojituma kwa dhati kuwatumikia wananchi.

Ndani ya kipindi cha takriban miezi tisa tangu kumalizika kwa Uchaguzi Mkuu wa 2010, Serikali mpya ya Manispaa ya Musoma Mjini imethibitisha ukweli huu licha ya changamoto nyingi zilizopo.

Serikali hii imeundwa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), baada ya kushinda kwa kishindo katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka jana. Meya, naibu meya na wenyeviti wote wa kamati za halmashauri, ikiwamo Kamati ya Fedha, Ardhi na nyinginezo, wote wametoka CHADEMA.

Hii ni kwasababu wananchi mbali na kuchagua mbunge kutoka CHADEMA (Vincent Nyerere), pia walikipa chama hiki maarufu mjini hapa kwa jina la “People”, madiwani wengi (11) huku CCM ikiambulia madiwani (4) na CUF (3).

Ziara yangu ya kiudadisi na kiupembuzi ilinikutanisha na wananchi wa kata mbalimbali za mjini Musoma, vijana, wazee na akina mama kwa kadiri nilivyoweza, ambapo kutoka kwao niliweza kupata taarifa na maoni huru kuhusu hali halisi ya wilaya yao ndani ya kipindi hicho kifupi cha miezi tisa. Aidha, iliniwezesha kutembelea na kushuhudia mafanikio yote ya kuonekana kwa macho, niliyoelezwa na wananchi.

Na hatimaye niliweza kupata taarifa za kitakwimu kutoka kwa Meya wa Mji huu, Alex Kisurura, Mbunge, Vincent Nyerere, pamoja na madiwani na baadhi ya viongozi wa serikali za mitaa bila kujali vyama vyao. Ziara hii ilinionyesha mambo kadhaa ya kupigiwa mfano yaliyopatikana ndani ya kipindi hicho kifupi tangu CHADEMA waingie madarakani, kama ifuatavyo:

Kwanza, kwa mtu aliyefika Musoma Mjini mwezi Oktoba mwaka jana (kabla ya kumalizika kwa Uchaguzi Mkuu), halafu akaingia tena hivi sasa, tofauti ya Serikali ya CCM iliyokuwepo na hii mpya ya CHADEMA inaonekana wazi wazi katika barabara za mitaa ya mji huu. Barabara nyingi kama za Kata ya Bweri, Nyamatare, Nyasho, Makoko, Mwisenge, Kigera na Buhare (eneo la Bima quarters) zilikuwa hazipitiki, na za kata nyingine chache zilipitika kwa tabu kwa sababu ya mashimo na makorongo mengi, lakini sasa zote zinapitika baada ya kufanyiwa ukarabati mkubwa na kuwekewa mitaro ya kupitishia maji pembeni ambayo haikuwepo kabisa, hivyo kuhakikisha haziharibiki mara kwa mara.

Katika elimu, serikali ya CHADEMA ilipoingia madarakani ilifanikiwa kufuta michango mingi isiyo ya lazima na kuipunguza ile iliyokuwa na umuhimu, ili kumpunguzia mwananchi mzigo wa gharama. Michango hiyo ambayo wakati wa utawala wa CCM ilifikia kiasi cha shilingi 140,000 hadi 250,000 kwa kila mwanafunzi, hatimaye imepunguzwa hadi kufikia wastani wa shilingi 52,000 hadi 62,000 tena pale tu kunapokuwa na ulazima.

Mathalani, mchango wa madawati uliokuwa shilingi 50,000 kwa kila mwanafunzi, lakini umepunguzwa hadi shilingi 5,000. Mbali na punguzo hilo, serikali ya CHADEMA pia ilichukua jukumu la kukarabati madawati kwenye shule zote za msingi. Na mchango wa maendeleo ya taaluma umepunguzwa kutoka shilingi 40,000 hadi shilingi 10,000.

Pia shule mpya (Shule ya Msingi Bukanga) imeanzishwa, ili kuwapunguzia adha ya kutembea umbali mrefu watoto wa eneo la Bukanga ambao wakati wa utawala wa CCM, walikuwa wanalazimika kutembea umbali wa takribani kilometa tatu kuifuata Shule ya Msingi Nyarigamba. Shule hiyo imeshaanza darasa la kwanza na inatumia majengo ya muda, huku ujenzi wa majengo yake ukisubiriwa kukamilika.

Na zipo shule nyingine tano za msingi ambazo zinajengewa maabara kwa fedha za Mfuko wa Jimbo. Sehemu ya fedha za mfuko huo pia inatumika kumalizia ujenzi wa majengo ya Sekondari kwenye Kata 10, ambayo Serikali ya CCM ilishindwa kuyakamilisha. Baraza la Halmashauri hii pia limeshaanza kutekeleza mpango wake wa kuzifanya sekondari za Morembe na Kyara kutoa elimu ya kidato cha tano na cha sita.

Viongozi wa CHADEMA pia wanawasomesha watoto yatima na wasiojiweza wilayani hapa kwa kuwalipia ada na gharama nyingine za elimu. Katika utaratibu huo waliojiwekea, Mbunge Nyerere, anasomesha watoto 70, Meya Kisurura watoto 100 na madiwani wa CHADEMA nao wana watoto wasiojiweza wanaowasomesha kwa fedha zao wenyewe. Kwa ujumla, kuna watoto wasiojiweza zaidi ya 200 wanaogharamiwa masomo na viongozi wa CHADEMA. Mbali na idadi hiyo, Serikali hii pia iliamua kuanza kuwalipia ada watoto 100 wasiojiweza, ambao serikali ya CCM iliwatelekeza kwa kuacha kuwalipia ada tangu mwaka 2008.

Katika nyanja ya afya, wananchi wa Musoma Mjini pia wana kitu cha kujivunia kwa kuiweka CHADEMA madarakani. Kwa kauli zao wenyewe na kwa ushuhuda wa macho na utashi wangu, ndani ya kipindi hicho kifupi tayari wodi ya watoto katika Zahanati ya Nyakato inajengwa na bado kidogo kukamilika.

Na chini ya usimamizi wa serikali hii, wodi kama hiyo pia inajengwa katika Zahanati ya Kigera kwa fedha za Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF).

Kwa mara ya kwanza katika manispaa hii, wazee, watoto walio chini ya miaka mitano na kina mama wajawazito wanatibiwa bure katika hospitali za serikali hapa Musoma.

Na Serikali hii ya CHADEMA imeshaanza kutayarisha vitambulisho kwa watu wa makundi hayo, ili kuhakikisha kuwa wanapata haki hiyo ya kutibiwa bure katika siku zote za maisha yao, haki ambayo walikuwa hawaipati wakati wa utawala wa CCM, licha ya sera za kiserikali kutamka hivyo.

Zahanati mpya zinaendelea kujengwa kwa kasi katika kata za Iringo na Buhare, pamoja na kuweka uzio kwenye Kituo cha Afya cha Nyasho na kwenye zahanati ya Bweri.

Kwa sababu ya ufisadi na usimamizi mbovu wa Serikali ya CCM, miradi mingi ya TASAF wilayani hapa kwa muda mrefu ilishindwa kukamilika na kubaki kusuasua, lakini sasa hali ni tofauti. Tayari ujenzi wa Zahanati ya Nyamatare uko mbioni kumaliziwa baada ya fedha za mradi huo kupatikana.

Aidha, msukumo wa Mbunge Nyerere na madiwani umewezesha kupatikana kwa gari jipya la kisasa la kubebea wagonjwa mahututi (Ambulance) kwa ajili ya kuwapeleka kwenye hospitali kubwa jijini Mwanza, huku mpango wa kufufua na kukamilisha ujenzi wa Hospitali Kuu ya Mkoa wa Mara, uliosuasua kwa miaka mingi mjini hapa, ukishughulikiwa kwa kasi.

Na katika hili, jitihada za Nyerere zimesaidia baadhi ya familia zilizohamishwa kwenye eneo linalojengwa hospitali hiyo, kulipwa fidia ya jumla ya shilingi milioni 100, ambayo walikuwa wakiidai kwa muda mrefu bila mafanikio.

Wakati wa utawala wa CCM wakazi wa Musoma Mjini walikuwa wakiteseka kwa shida kubwa ya maji, licha ya kuwa mji huu umezungukwa na Ziwa Victoria.

Hii ni kwasababu, kwa zaidi ya miaka 30, Serikali ya CCM haikufanya kazi ya kukarabati miundo mbinu ya mabomba ya maji, ambayo sasa imechakaa kiasi cha kuwa na uwezo wa kusambaza maji kwa wananchi 50,000 tu, wakati Musoma yenyewe ikiwa inakadiriwa kuwa na watu takriban 181,000. Serikali mpya imeamua kulishughulikia kwa kasi tatizo hili linalogusa moja kwa moja uhai wa binadamu, na sasa mradi wa maji utakaogharimu takriban shilingi bilioni 50 unaanza kutekelezwa chini ya usimamizi wake.

Wakati mradi huo mkubwa ukianza, baraza la halmashauri limekwisha kuidhinisha fedha kwa ajili ya kutekeleza mradi wa kupeleka maji kwenye Kata ya Buhare, iliyo katika shida kubwa. Na tayari mpango wa uchimbaji wa visima vya dharura hivi karibuni upo mbioni kuanza, hususan kwenye maeneo yenye shida kubwa sana ya maji kuliko maeneo mengine. Mipango ya mbunge, meya na madiwani, ni kuhakikisha shida hii inakwisha kabisa katika maeneo yote kwani maji ya Ziwa Victoria yapo, kazi iliyoishinda CCM ni kuyavuta tu.

Katika nyanja ya ajira, kwanza serikali ya CHADEMA ilipoingia tu madarakani hapa Musoma, ilifuta ushuru uliokuwa ukitozwa kwa wafanyabiashara ndogondogo za uchuuzi kama ule uliokuwa ukitozwa kwa kina mama wanaouza mbogamboga, matunda, dagaa na bidhaa nyingine ndogondogo za kujitafutia riziki, lengo likiwa ni kuwapa nafuu ya maisha wananchi hawa.

Pili, kwa lengo la kuwajengea wananchi mazingira mazuri ya kujipatia kipato, serikali hii imeweza kukarabati na kulifufua Soko la Kamnyonge ambalo lilisimama tangu mwaka 1986.

Masoko mengine yanayofuatia katika mpango huo, ni Soko Kuu la Musoma, Soko la Mlango Mmoja, Nyasho, Soko la Samaki (Makoko), Nyakato na Soko la Mwalo wa Mwigobero ambalo litaanza kukarabatiwa kwa kushirikiana na Mamlaka ya Bandari Tanzania.

Tatu, vijana waendesha pikipiki (bodaboda) waliokuwa wanalalamikia utaratibu wa kulipa kodi ya shilingi 95,000 kwa mkupuo mmoja kwa mwaka, sasa wamepewa nafuu ya kutakiwa kulipa kodi hiyo kidogokidogo, ilimradi tu mwaka usiishe bila mhusika kukamilisha malipo ya kiwango hicho cha kodi.

Nne, vibanda vya biashara vya manispaa hii vilivyokuwa vinamilikiwa na watu wachache wakati wa CCM, sasa vimetaifishwa na serikali ya CHADEMA na kugawanywa kwa usawa kwa wananchi wengi zaidi wakiwemo walemavu, ili kuwapa fursa ya kujitafutia mkate wao wa kila siku.

Tano, serikali hii mpya pia inasimamia ujenzi na upanuzi wa stendi kuu ya mabasi makubwa yaingiayo Musoma (Stendi ya Bweri), ili iweze kufanya kazi kwa saa 24 na kwa ufanisi zaidi na hivyo kuipatia manispaa mapato ya kutosha kwa ajili ya miradi mingine ya maendeleo, na wakati huo huo ikitazamiwa kutoa fursa nzuri kwa wajasiriamali wa mji huu kujitengenezea kipato kwa kufanya biashara.

Sita, nimeshuhudia kukamilika kwa ujenzi wa kivuko kikubwa ambacho kitafungua safari za ziwani kutoka Musoma hadi Bunda. Mradi huu unatarajiwa kuchochea maendeleo ya shughuli za kibiashara na kiuchumi baina ya wilaya hizi mbili zinazozungukwa na Ziwa Viktoria.

Saba, serikali hii imeamua kuwa asilimia 10 ya mapato ya manispaa yanayopaswa kushughulikia maendeleo ya vijana na kina mama, yatumike kuanzisha miradi midogomidogo ya pamoja, badala ya kutoa mikopo isiyo na tija ya shilingi elfu 50 kwa mtu mmoja mmoja.

Kwa mujibu wa viongozi wa serikali hii, baadhi ya miradi ambayo iko mbioni kubuniwa kwa kuwashirikisha wananchi wenyewe ni pamoja na kuanzisha kiwanda kidogo cha kutengeneza biskuti za viazi, ununuzi wa mashine za kutotolea vifaranga, kutengeneza chakula cha kuku, kutengeneza chaki, na kuviwezesha baadhi ya vikundi vya wavuvi na wafugaji kuuza samaki na maziwa ya kutosha kwenye viwanda viwili vilivyopo mjini hapa.

Katika nyanja ya utawala bora, meya, mbunge na madiwani wa manispaa hii, wamejiwekea utaratibu wa kufanya mikutano ya hadhara ya mara kwa mara na wananchi ili kuwapa mrejesho wa kazi wanayoifanya na kupokea kero na matatizo mapya kutoka kwao. Pia viongozi hawa kila mmoja ameshawatangazia wananchi namba yake ya simu ya mkononi, kwa ajili ya kutoa kero na matatizo yao kwa urahisi ili yapatiwe ufumbuzi wa haraka.

Na wakati huo huo serikali hii inaendelea kujenga ofisi za watendaji kata, ambazo hazikuwepo kwenye kata mbalimbali mjini hapa ili zitumiwe na wananchi kama fursa ya kuwasilisha kero, matatizo na malalamiko yao kwa diwani, mbunge au halmashauri yote.

Viongozi wanahakikisha kuwa asilimia 20 ya fedha za mapato ya manispaa inabaki kwenye ofisi za serikali za mitaa, ili kuhakikisha kuwa ofisi hizo zinawahudumia wananchi bila kuwatoza chochote. Kabla ya hapo ulikuwa huwezi kupata barua ya utambulisho kutoka ofisi ya mtaa, au kutatuliwa mgogoro wako, bila kuchangia fedha kama shilingi 2,000 ya karatasi au fedha za kuwaita wajumbe kwenye vikao vya usuluhishi (michango hii haramu bado ipo maeneo mengi nchini ikiwemo kwenye ofisi za serikali za mitaa za jijini Dar es Salaam).

Nilipata bahati ya kupitia pia ripoti mbalimbali za kifedha kuhusu manispaa hii, kubwa nililobaini ni kwamba serikali hii mpaka sasa imeshafanikiwa kudhibiti matumizi makubwa na ya anasa ya fedha za umma.

Mathalani, idadi ya semina, warsha na safari za nje ya manispaa zilizokuwa zikifanywa na meya, naibu meya na madiwani wa CCM wakati wa enzi za utawala wao, sasa zimedhibitiwa kwa kiasi kikubwa, na badala yake fedha hiyo nyingi ndiyo inayotumika kutekeleza kwa kasi miradi mingi ya maendeleo ya wananchi.

Changamoto zipo nyingi ikiwemo ya uhaba wa fedha za kutekeleza miradi ya maendeleo, lakini bado serikali hii inaonekana kufanya mengi ya kuvutia ndani ya kipindi kifupi tu cha miezi tisa.

“Tulipokea mji huu ukiwa katika hali mbaya sana. Wakati CCM imetumia miaka 50 kufanya vitu vichache na visivyoonekana dhahiri, sisi mpaka sasa tumeweza kufanya vitu vingi ndani ya miezi nane tu, na bado tuna uhakika wa kufanya makubwa zaidi ndani ya miaka mitano.

Siri ya mafanikio haya, ni uadilifu, uwajibikaji na kutekeleza kwa vitendo falsafa ya CHADEMA ya “nguvu ya umma”, ambapo kwa falsafa hiyo, tumeweza kuiweka serikali hii mikononi mwa wananchi wenyewe, kwa kuwafanya kuwa ndio waamuzi wa mwisho wa nini wanataka kifanyike, huku tukiwapa fursa ya kufuatilia na kusimamia kila kinachofanyika.” (Kauli ya Vincent Nyerere).

Hakika huu ndio ufunuo wa CHADEMA kwa Watanzania kutoka Musoma, kwamba, “Maendeleo yaliyoshindikana ndani ya kipindi kirefu cha ufisadi, uzembe na usanii, sasa yanawezekana ndani ya kipindi kifupi cha uadilifu, na uwajibikaji”.

SOURCE: Tanzania Daima Newspaper- Wednesday October 19, 2010

Friday, October 21, 2011

Successful Training: Thanks to MISA -TAN & VIKES:

Hi, the World.

This is to confess that, the three -days training on investigative internet journalism has been very successful to me and am sure to all participants.

On this third day, we went deep to a Journalistic Research Via Internet, establishment of internet links (within blogs in particular) and off-course learnt more on how to report internet investigated stories.

There were so many lessons learnt from the facilitator and infact from the deliberations of all participants, some of them are as follows;

First, we journalists have learnt how to employ effectively the theories and tools of search engines for investigative journalism.

Second, the effective use of internet has proved to be the fastest and easiest way of conducting investigative topics for our journalistic coverages. For instance, now I can employ all the search options in the google, including Satellite searches, something that I was not familiar with before.

Third, now we are aware that lots of information and facts, is available in the websites and other internet social media, and just in case, something searched not found, the investigative journalist can ask and share with other people via internet, the real facts and information, that is looking for.

Fourth, Mr Peik Johansson (the facilitator), introduced to us a list of useful websites and social media, which can be applicable into our daily journalistic life.

Fifth, as a result of this training, every participant now has became a blogger, and this Kinabo Forum (Freeing Ideas for Free Nations) is a real evidence.

Sincere thanks to the MISA-TAN, the VIKES, and Mr Peik (our facilitator) in particular.

Lord's Resistance Army: The Most Confusing Rebel Group that US want be suppressed

By Edward Kinabo

Hi, the World.

How tough is the Uganda's Lord's Resistance Army, such that President, Barack Obama announced to help President Yoweri Museveni, to suppress it? What exactly this rebel group fighting for in Uganda, South Sudan, Democratic Republic of Congo, and in parts of Central Africa?

It was made clear last week that 100 US soldiers will be deployed soon to the East African country, to coach the native soldiers on how to suppress completely the long undefeated rebel army, which has survived over 24 years, since their leader Joseph Kony formed it.

I believe that deploying these U.S. armed forces furthers U.S. national security interests and foreign policy, and will be a significant contribution toward counter-LRA efforts in central Africa,"wrote Obama in his letter to John Boehner (Speaker of the US assembly)as quoted by BBC.

The Obama's letter content mainly alleged the rebel group to have violated human rights and victimized more than 380,000 people. The very same claims that said by US when sent troops in Iraq and into many other countries of the world.

Throughout the years, the LRA has been ambushing civilians, brutalizing and taking them as sexual captives (women)and forcing boys to be new soldiers in fighting against Uganda government, people of South Sudan, Central African Republic and the Democratic Republic of Congo.

Whats more interesting about this rebel army, is the confusing mission and ideology they are fighting for? Throughout different sources of information and news, nobody knows for sure yet, what is a focused objective of this rebel group.

Majority think Joseph Kony's group is fighting for power, that is, to overthrow the Museveni's government and start a new christian regime, whose ideological constitution will be the Ten Commandments of God found in the holy bible.

But other analysts say no, this is not a christian movement. If so why are making sins of violating human rights like raping, killing, and enslaving women for sexual purposes? And here they refer to the John Ochola's testimony for BBC in 2006, who was chopped hands,ears and nose by the LRA, such he is know a handcapped man.

Instead, they say the group is fighting to restore the Acholi tribe' nationalism and make it govern Uganda. Acholi is the tribe of Joseph Kony ( the leader).

However, if that the case, why fighting in more than one place -Uganda, South Sudan, Democractic Republic of Congo and Central Africal. How can Acholi's nationalism be restored everywhere, in the four countries?

No matter what, this is a very confusing rebel group, with a very confusing ideological mission, ever happened in Africa and the World at large. Lets wait for US mission, may be the real mission of LRA will be revealed.

Thursday, October 20, 2011

Journalistic Research via Internet: Lessons from Day Two of MISA-TAN and VIKES Training

Hi, the World.

The second day of the MISA TAN and VIKES' Training on Investigative Internet Journalism, started for participants writing the review of Day one in their blogs. Under that assignment,earlier today I posted to my blogs the review tittled "Investigative Journalism with Internet".

After that, Mr Perk Johanson, brough us into a practical journalistic research via the internet world. Then we attempted about ten exercises measuring our understanding on the use of internet tools and theories of search engines.

Here we surveyed several options of searching facts from internet in a simple way, especially on how to employ different search options from the google, as Maps, News, Images, Translate, Satellite etc.

The major lesson rose from this topic was that, "first give yourself time to think on how you are going to search before rushing to the website. Failure to do so will end up finding yourself consuming more time, than you had to".

Again, the same exercise gave us the foundation of attempting special questions, throughwhich we had to undergo investigative journalism by internet, then writing and publishing the researched stories on the blogs. And from this I managed researching and publishing the articles titled "LEILA LOPES: Why She became famous woman of the World?

The training will continue and end up tomorrow evening

LEILA LOPES: Why she became famous woman of the World?

By Edward Kinabo

She hits the headlines of international media, both in electronic and print ones and actually has became the subject matter of discussion among many visitors of internet social forums, facebook, twitter and the like, through which sensational stories about her, are shared.

Yes she won the title, that is, Miss Universe 2011, contested in Sao Paul Brazil on September 12, 2011; Yes she comes from our beautiful marginalised continent (Africa); But whatever the case, this couldn't be enough to make the 25 years old Lopes (from Angola) - the most famous woman of the month or even the day.How could it be while we all know for sure that she is not the only miss universe the world has ever had nor Africa is proud off?

In fact, she is the 60th winner of the same worldwide contest and the fourth one from Africa, preceeded by other African winners emerged from South Africa, Namibia and Botswana. What's peculiar facts then surrounding her very fast overgrown fame, especially in this preliminary moments after the victory?

I couldn't handle my curiosity in getting to know more about this lady, and therefore my searches from several websites like ibtimes.com, the wikipedia, ended up finding the followings;

That, Miss Lopes is condemned to have forged documents which enabled her justify her residency in United Kingdom,showed to have studied at the University Campus Suffolk of Ipswich town. Therefore, qualified to
participate the Miss Angola beauty contest for the Angolan diaspora of UK on October 8, 2010,where she won.

Her victory in England led her to partcipate and win the Miss Angola beauty contest held in Luanda two months later, which then gave her a ticket of participating the Miss Universe Contest condected in Sao Paul.

Again, Miss Lopes is alleged to have bribed some judges in UK,otherwise she couldn't win the ticket to Angola contest nor pass through to the Sao Paulo held miss universe contest.

However, there is no much evidence yet about her forgery and fradulent deeds, but that is what is discussed and shared strongly throughout the World. What's more, the organizers of Brazil Miss Universe have confirmed that "Lopes will loose her crown if the allegations will be proved true"

There others who say, Miss Lopes didn't deserve to win, claiming that she underwent costimetic surgery to fake her beauty.

But when interviewed some days later, She said is satisfied in the manners her God created her, adding that the secrets of her beauty is rooted in her unique smile, the way she take good care of her skin and the diets.

All these allegations, has turned up Leila Lopes to be a Scandalous Miss Universe, and hence the most famous woman of the World in the last month.

Investigative Journalism with Internet:Day One of the MISA-TAN and VIKES Training

By Edward Kinabo

Hi the World.

Please let me (Journalist from Tanzania Daima Newspaper) share with you this crucial opportunity of being part of the Tanzanian Journalists attending a capacity building workshop on investigative journalism whose main focus is the use of internet for such purpose.

The three -days training conducted by the Media Institute of Southern Africa, Tanzania Chapter (MISA-TAN) in collaboration with VIKES (Finnish Foundation for Media, Communication and Development) started yesterday October 19, 2011, at Tanzania Global Learning Center (TGDLC) in Dar es Salaam.

Under the facilitation of Mr. Perk Johanson (from VIKES), we were introduced to the different concepts of Investigative Internet Journalism. Now, I can describe it as the process of searching deeply for unknown information by use of internet, in order to make it known through media (be it electronic or print ones), making it easily understood and useful for the public interest.

The use of internet social forums like facebooks, twitter, social websites like Jamii Forums of Tanzania and many other, was suggested to be the easiest means of investigative journalism in Tanzania, as many people can share and contribute whichever they know on the issues which is under investigation.

It was agreed by the participants that investigative journalists can publicize the subject matter of their investigations openly in these forums and request visitors to offer facts and information they know.

By so doing, the investigative journalist will be able to access a lot of desired information of which would take long time or would be difficult to get if one could strive for it all alone.

The journalist can also offer his or her email address in the internet forum, for the information to be sent directly by every respondent, without giving them loop holes of knowing each other, if confidetiality is very necessary.

We got a chance of visiting some popular websites like the Wikileaks, Dispatchonline, Fair (that is Forum for African Investigative Reporters) and the Center for Investigative Reporting.

Also visited various publications  and articles like, "Investigative Journalism Manual" and "How investigative journalism is prospering in the age of social media". These can be accessed by searching in the www.google.com and has a lot to educate on how internet use makes investigative journalism much easier.

The day one of the training ended up for every participant to learn how to establish their internet forums popularly known as blogs. It was from this interesting topic that I managed to open up this "KINABO FORUM" whose address is kinaboforum.blogspot.com.

I hereby welcome the world to share together useful perspectives for the development of humankind,in the context of socio-economic, civil rights;and political issues, via the KINABO FORUM. The training continues today.